NILILALA NA MAITI 20 ILI NIOLEWE NA RAISI SEHEMU YA 3

Mtunzi: JONS JONAS

Simu: +255 613 321 991

Ilipoishia…

“Adela mwanangu umekuja?”

Aliongea yule mama wa kwanza kabisa. yule alioniambia kuwa ni kiongozi wao na atanipangia kazi ya kulala na maiti ishirini.
“Ndio mama”

“Umependeza mwanangu! Hivyo ndivyo mabinti wakike wanavyoishi huku kwetu.

Si umeniona hata mimi sinma maziwa? Yaani huku hayana kazi maana kama mimba hatupati sasa miziwa inafanya kazi gani?”

Songa nayo…

************************************

Nilijiangalia mara mbili mbili kifuani mwangu kwa hasira ya hali ya juu.

Yale maziwa madogo dogo na ya kumvutia kila mwanaume sasa yalikuwa hayapo tena katika kifua changu. Yametolewa na wale wazee wachawi wenzangu.

Niliumia sana lakini kwa kuwa tayari nilishakubaliana na nguvu ya kiuchawi ilinibidi yatolewe.

“Adela?”

“Abee mama!”

“Kuanzia sasa usiniite mama, mimi siyo mama yako sawa?

Mbona mimi sikuiti mwanangu na kuita Adela? Nataka uniite Sophia ama sophy, tumeelewana Adela?”

“Ndio sophy nimekuelewa.”

“Haya sogea karibu yangu hapa nilipo kisha nikumbatie kwa nguvu.”

Aliongea yule Sophy kwa sauti ya ukali akinisisitizia kwa mkazo.

Nilitahamaki maneno yake ya ukali lakini nilijikuta naingiwa na moyo wa subira.

Moyo wa kuvumilia yote nionayo na nisikiayo.

Mwili wangu bado ulikuwa haujakamilika kabisa kwa uchawi kwani nilianza kuhisi woga woga ukininyemelea kila muda niliokuwa nikiongea na Sophy.

Hata aliponisihi nimsogelee na kumkumbatia bado nilikuwa nikimuogopa.

“Hivi unanisikia Adela ninachokuambia? Au unataka nikurudishe kule kwa wazee ulipokuwepo wakakuchezee tena mwili wako?”

“Hapana mama, anhh nisamehe!!. Hapana Sophy!”

Kwa uoga uliochanganyikana na aibu kwa mbali ilinibidi nimsogelee na kisha nichukue mikono yangu na kupitisha mabegani mwake kwa lengo la kumkumbatia kama alivyohitaji.

*******

Baridi kali lilikuwa likiendelea kuusumbua mwili wangu. Kiza kinene kiliyashinda macho yangu angavu. Macho yenye nguvu ya kuangaza popote sasa yakawa hafifu.

Hafifu kwa kutoweza kuona vizuri mbele wala nyuma. Nikajikuta nikiwa juu ya mti mkubwa sana. Mti aina ya mbuyu uliopukutika majani yake na kuwa mkavu.

Nafsi yangu iliuliza moyo lakini akili ilibaki kutokujua na kukataa kuujibu moyo juu ya kinachoendelea.

Sauti za ndege aina ya popo na bundi ndizo zilienea zaidi. Mwili wangu haukuwa mwili wa kawaida tena kutokana na kujikuta nimezungushiwa shanga na hirizi karibu mwili mzima na mikononi nikiwa nimefungwa vitambaa vyekundu.

Pembeni yangu alikuwepo Sophy akiwa amebebelea ungo mkubwa uliokuwa umejaa vibuyu, vidole vya watoto, masikio ya watu wazima pamoja na mikia.

Sikuelewa vizuri ilikuwa ni mikia ya mnyama gani kutokana na mikia kuwa mirefu sana.

Sophy alionesha kufurahi jambo akinitazama usoni mwangu.

“Adela sasa kazi yetu inaanza rasmi sasa hivi.

Na hapa nilipo nipo kwa ajili ya kukuonesha tu utakavyokuwa unafanya na siku nyingine utakuwa unakuja peke yako mpaka utakapomaliza zoezi la kulala na maiti zote ishirini, umenielewa Adela?”

“Nimekuelewa Sophy”

Nilijibu kwa kujiamini kana kwamba tayari ni mchawi aliyekamilika.

Baada ya hapo Sophy akachukuwa Mikia miwili na mmoja wapo akanikabidhi kisha akaniamuru ule mkia niwe nauchovya kwenye kibuyu kuna nguvu zetu za kutulinda tusionekane na wala tusikamatwe na mtu yeyote na hata tukikutana na mchawi ambaye hayupo katika himaya yetu asiweze kutudhuru.

Nilifanya hivyo pamoja na Sophy naye alikuwa akifanya hivyo hivyo huku tukishuka kwa kuteleza chini ya mbuyu taratibu.

Tulipofika chini kabisa nilishangaa kukutana na makaburi mengi yakiwa yamejipanga.

“Adela?”

“Abee Sophy?”

“Haya ni makaburi ya Mwananyamala na kwa kuanza chukua hiki kibuyu kitakuwa kinakuongoza.

Unapita mstari huu wa makaburi huku ukiyapandia juu yake mpaka kule mwisho na ukijiona mzito unashindwa kwenda mbele ujue hilo ni kaburi la mwanaume ambaye amezikwa leo leo.
Haya tuanze mimi nipo nyuma yako taratibu”

Nilijikuta nauvaa moyo wa kijasiri na wakiuchawi. Woga uliniyeyuka ghafla na kuvaa ngozi ya kichawi tena yule mchawi aliyekubuhu kwa uchawi.

Nilianza kupiga hatua nikifuata mstari wa makaburi kwa kuyakanyaga juu yake.

Nilifanya hivyo kwa zaidi ya makaburi sita lakini nilipolikaribia kaburi la saba nilishangaa mwili wangu kama kutetemeshwa.

Ganzi! Ndio ganzi mithili ya shoti ya umeme ilikuwa imeninyuka katika miguu yangu vilivyo.

Nilitetemeka na kutaka kuanguka mpaka chini.

“Adela? Nini tena unafanya? “

“Sophy nashindwa kutembea, nashindwa nivute?”

“Hivi unajua kuwa ilo sio kaburi unalotakiwa kulichimba leo. Na kaburi hilo uliokanyaga ni la zamani sana.

Ukiona miguu inatetemeshwa ujue hilo kaburi litakuwa la mchungaji ama kiongozi wa kanisa au msikiti.

Mara nyingi huwa inatutokea tukiwa katika mawindo yetu haya. Sasa si unaona na maua kabisa yanaonekana yamewekwa leo.

Watakuwa walikuja kulisafisha na kuliombea mchana au asubuhi”

“Ndio”

“Lazima utakuta waliweka maji yao ya Baraka sambamba na kuliombea lakini usijali Adela,
dawa zetu zina nguvu zaidi yao twende.”

Nilishangaa nakuwa mwepesi kwa mara nyingine. Sophy alinivuta mkono wangu sambamba na kunipokonya kile kibuyu nilichokuwa nacho na kubakiwa na mkia pekee.

Niliongozana naye kwa zaidi ya makaburi kumi na moja akasimama.

“Adela umepaona hapa?”

“Ndio”

“Hapa kibuyu kimekataa kusogea na hata mkia pamoja na shanga zangu za kiunoni nilizokuwa nazo zinacheza cheza sana. Na wewe umehisi hilo?”

“Mimi zinaniwasha sana na mkia nilioushika unajitingisha wenyewe.”

“Basi hapa ndipo penyewe. Kama ukiona kibuyu kinacheza peke yake ujue hilo ni kaburi la mwanamke achana nalo.

Lakini kama utaona kibuyu pamoja na mkia na hizo shanga ulizonazo zote zinacheza cheza ujue hilo ni la kiume na hata si unaona kaburi lilivyo jepesi pamoja na mchanga wake uliofukiwa inaonyesha dhahiri kuna maiti ya kiume tena imefukiwa leo leo.

Haya unatakiwa uweke kibuyu hapo pembeni ya msalaba wao hili nguvu yetu ya kichawi iweze kushinda na baada ya hapo utatumia mikono yako kuchimba hili kaburi.”

Ule woga wote niliokuwa nao ulishafutika toka nimekatwa maziwa yangu na kuwa mchawi kamili.

Roho ngumu na ya kichawi ndio ilionitawala katika halmashauri ya kichwa changu. Kwa haraka zaidi nilifanya kama nilivyoelekezwa na Sophy.

Nilichimba kaburi kwa kutumia mikono yangu.

Nilishangaa nguvu za ajabu nilizokuwa nazo za kuweza kulifukuwa kaburi refu kwa muda mchache, nilijikuta nimeshafika umbali mrefu sana.

Niligeuza macho yangu kuangalia juu nilipotoka lakini sikuweza kumuona Sophy japokuwa kulikuwa na mwanga wetu wa kichawi uliosaidiana na mbalamwezi.

Nikaendelea na kilichonileta hapa kaburini. Baada ya kuendelea kuchimba kwa muda kidogo nilikutana na mbao mbao.

Akili yangu ikajibizana na mdomo na kutambua kuwa ilikuwa ni jeneza. Nilishika mbao zake kwa nguvu zote na kuanza kulifungua.

Nilifanikiwa kulifungua japokuwa nilikutana na harufu kali sana. Mara nyingi harufu za kichawi hufanana sana na zile pafyumu za kupulizia maiti hivyo hazikuniathiri pua zangu ama mimi mwenyewe.

“Umependeza!!”

Nilijikuta natoa mdomo wangu nakuusemea moyo huku nikiangalia ile maiti kwa jinsi ilivyokuwa imevalishwa suti nzuri na ya kuvutia.

Nikalitoa bao lote lililokuwa limefunikiwa kwa juu. Nikaanza kumvua nguo zake taaratibu kuanzia tai, koti la suti na kisha nikamalizia suruali yake mpaka akabakiwa uchi kabisa.

Mwili wake ulikuwa umesinyaa sana nadhani ilitokana na kukaa mochwari kwa muda mrefu ama alikuwa akiugua sana hilo sikulijali Adela mimi zaidi ya kuendelea kumvua nguo.

“ Mlambe lambe kuanzia kifuani, mdomoni, na kisha umnyonye sehemu zake za siri. Ukimaliza ufanye naye mapenzi kwa kumlala juu yake kama wafanyavyo wapenda nao huko duniani!”

Sauti mbili mbili zilizochanganyikana na sauti ya Sophy zilikuwa zikitikisa ngome ya masikio yangu.

Nikataharuki! nikaanza kuzubaa sasa. Kadiri nilivyokuwa nikizubaa kwa kuzisikiliza sauti zile zilipotokea ndipo nazo zilikuwa zinaongezeka na kurudia maneno yale yale.

Kwa takribani dakika tano nzima zile sauti ziliongezeka mara kumi ya pale kwani niihisi watu wengi sana wananiambia maneno yale.

Mwili wangu ulishtuka kama vile ulipigwa na radi. Nilijikuta ghafla nikisisimka sambamba na furaha.

Nikaanza taratibu kulamba usoni ile maiti na mikono yangu nikiitumia kumtoa pamba zake puani na masikioni mwake.

Niliendelea kumnyonya mdomoni mwake ulimi wangu nikiutelezesha mpaka kifuani mwake.

Nikiwa bado katika hali ya kumnyonya ghafla nikashangaa ile maiti kushtuka. Nikataharuki!

nikainuka na kuiangalia vizuri, nikashangaa jicho moja la maiti hii likifumbua na kunitazama kama inataka kunisemesha jambo.

Nikabaki nimetulia kama mtu aliyegongewa misumari katika mbao au bati.

“Sophhhhhyyyyy??”

Uzalendo ulinishinda kabisa nikabaki nikitoa sauti ya ukali na ya juu kabisa kumuita Sophy.

Sophy yule niliekuja naye huenda nilikosea masharti au nguvu za kichawi zimeniishia.

Lakini sikuambulia msaada wowote zaidi ya ile sauti nilioitoa kumuita Sophy ikinirudia mwenyewe mithili ya mwangi wa sauti katika mapango marefu na yenye giza.

***********************

**** Unavyodhani Adela atanusurika hapo na hiyo maiti? Vipi kuhusu Sophy?, atakuwa wapi au amerudi kule kwa wachawi wenzake akamuacha Adela? Nini hatma ya maisha ya Adela?

**** Simulizi ndio kwanza imeanza, tegemea utamu zaidi kila itakapokuwa inaendelea. Gonga LIKE zikifika 200 naachia tena nyingine.

**** ANGALIZO ****
Hairuhisiwi kusoma kwa mtu ambaye anajijua ni muoga. Ukijihisi kila unaposoma mapigo ya moyo yanakwenda kasi, tafadhali acha. Pia si vizuri ukawa unasoma katika mazingira ambayo upo peke yako ama unaishi peke yako katika nyumba hasa nyakati za usiku. Na siyo vizuri kusoma ukiwa maeneo ya beach,chini ya miti mikubwa ama karibu na makaburi, hospitali zenye vyumba vya kuhifadhia maiti ama milima ni hatari sana.